Mkurugenzi Kinga na Elimu ya Afya Dr Salum Slim  Mohammed  ameupongeza  Uongozi wa Chuo Kikuu Cha Taifa Zanzibar SUZA  kwa kuendelea kufanya tafiti mbalimbali za Afya   ambazo zinasaidia wizara katika  kuboresha  Afya nchini
Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku 3 ya mradi wa Uimarishaji wa Huduma jumuishi za VVU, TB na Malaria wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua   kwa baadhi ya wakuu wa vituo vya Afya Unguja na Pemba
Nae Mkuu wa Skuli ya Afya na Sayansi za Tiba  ya Chuo Kikuu cha Taifa Cha Zanzibar  Dkt Salma Mahmoud Abdi  amesema mradi huu utasaidia kupunguza vifo vya mama na watoto  na kusaidia kuzuia msongo wa mawazo  kwa wazazi waliojifungua.
Mradi huu umefadhiliwa na Global Fund  kwa kushirikiana na Liverpool School of Tropical Medicine cha nchini Uingereza pamoja na Chuo Kikuu Cha Taifa Zanzibar (SUZA).